zeno
Create a Station
Explore
Religious
Music
News
Podcasts
Bible
By Genre
By Location
By Language
Download App
Toggle Sidebar
zeno
United Nations
Habari za UN - Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu
Daily News
Swahili
Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu
Website
Episodes
100
24 June 2026
Papa Leo XIV: Juhudi na mshikamano wa kimataifa ni kiini cha kutokomeza njaa
Katika kipindi ambacho idadi ya watu wanaokabiliwa na njaa duniani inaendelea kuongezeka kutokana na migogoro, mabadiliko ya tabianchi na changamoto za kiuchumi, kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Leo wa Kumi na Nne (Leo XIV), ametuma ujumbe wa mshikamano kwa kutembelea makao makuu ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani, WFP, mjini Roma nchini Italia wiki hii. Ziara...
2 min
24 June 2026
UN yathibitsha zaidi ya matukio 500 ya ukatili wa kijinsia nchini Sudan
Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Binadamu, OHCHR, imetoa ripoti kuhusu ongezeko kubwa la ukatili wa kingono unaohusiana na mzozo nchini Sudan tangu mapigano yalipoanza zaidi ya miaka mitatu iliyopita. Ofisi hiyo imekumbusha jumuiya ya kimataifa umuhimu wa kuhakikisha haki na uwajibikaji vinapewa kipaumbele wakati juhudi za kusitisha mapigano na kutafuta suluhu ya mzozo huo zikiendelea. Tupate...
2 min
24 June 2026
24 JUNI 2026
Hii leo jaridani tunaangazia usalama wa mabaharia katika Mlango Bahari wa Hormuz, ongezeko kubwa la ukatili wa kingono unaohusiana na mzozo nchini Sudan, na ujumbe wa Papa Leo wa Kumi na Nne (Leo XIV), kuhusu ongezeko la njaa duniani.Shirika la Umoja wa Mataifa la Usafiri wa Baharini (IMO) limetangaza mpango wa kuwaondoa zaidi ya mabaharia 11,000 waliokwama katika Mlango Bahari wa Hormuz kufuatia...
9 min
24 June 2026
IMO yatangaza mpango wa kuwaondoa mabaharia waliokwama Hormuz
Shirika la Umoja wa Mataifa la Usafiri wa Baharini (IMO) limetangaza mpango wa kuwaondoa zaidi ya mabaharia 11,000 waliokwama katika Mlango Bahari wa Hormuz kufuatia makubaliano ya amani kati ya Iran na Marekani yaliyolenga kurejesha usalama wa usafiri wa baharini katika eneo hilo. Anold Kayanda amefuatilia hatua hiyo. Karibu Anold utufahamishe zaidi.
3 min
23 June 2026
Jifunze Kiswahili: Maana za neno "TANUWINI"
Katika kujifunza lugha ya Kiswahili hii leo mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA anafafanua maana za neno "TANUWINI"
23 June 2026
23 JUNI 2026
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayoturejesha hapa makao makuu ya Umoja wa Mataifa ambapo Leah Mushi ameketi chini na Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Nassriya Nassir Ali akieleza safari yake ya uongozi wa nafasi za umma kupitia mkalimani wake wa lugha ya alama Tusajigwa Ernest. Pia tunakuletea Muhtasariw a habari na jifunze Kiswahili.Janga la tabianchi linakaribia...
22 June 2026
22 JUNI 2026
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina. Hivi karibuni Shirika la Umoja wa Mataifa la Kupambana na UKIMWI, UNAIDS kupitia ripoti yake mpya limeonya kuwa kupungua kwa ufadhili wa kimataifa na uwekezaji mdogo katika huduma za kinga dhidi ya Virusi vya UKIMWI, VVU kunaweza kufuta mafanikio yaliyopatikana katika mapambano dhidi ya UKIMWI duniani.Katika hatua za mwitikio wa kitaifa, wiki iliyopita,...
9 min
19 June 2026
19 JUNI 2026
Hii leo jaridani tunaangazia wito wa UN wa kulinda mamilioni wa wakimbizi kote duniani, masuala ya kijinsia Zanzibar nchini Tanzania, na ripoti mpya ya Katibu Mkuu wa UN kuhusu watoto katika maeneo ya machafuko imeonesha hali ya kutisha duniani.Kuelekea maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Wakimbizi kesho Juni 20, viongozi wa Umoja wa Mataifa wametoa wito wa kuimarishwa kwa mshikamano na hatua za...
9 min
19 June 2026
UN yataka dhamira mpya wakati takriban wakimbizi milioni 42 duniani wakiendelea kuhitaji ulinzi
Kuelekea maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Wakimbizi kesho Juni 20, viongozi wa Umoja wa Mataifa wametoa wito wa kuimarishwa kwa mshikamano na hatua za kimataifa za kuwalinda mamilioni ya watu waliolazimika kuyakimbia makazi yao kote duniani kutokana na vita, vurugu na mateso. Anold Kayanda amefuatilia na kutuandalia taarifa ifuatayo.
2 min
19 June 2026
Mauaji na majeraha ya watoto yafikia kiwango cha kutisha duniani - UN
Ripoti mpya ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu watoto katika maeneo ya machafuko imeonesha hali ya kutisha duniani. Takribani watoto 24,174 waliuawa, kujeruhiwa, kulazimishwa kujiunga na makundi yenye silaha, kubakwa au kuathiriwa kwa namna nyingine na ukiukwaji mkubwa wa haki katika maeneo yenye mizozo mwaka 2025. Leah Mushi amemsikiliza Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa...
2 min