About
Leo katika kujifunza lugha ya Kiswahili tunakwenda Burundi, ukanda wa Maziwa Makuu barani Afrika na mchambuzi wetu ni Ntahombaye Hussein, Mwenyekiti wa Chama cha Wanahabari wa Kiswahili nchini Burundi, CHAWARUNDI. Anafafanua maana ya neno, “KUROWA”.Hiki ni kitenzi kikimaanisha kuvua samaki na nomino yake ni mroaji.Sentensi: Mroaji ameenda ziwa Tanganyika kuangalia iwapo atapata kitoweo cha samaki.Hii inamaana mroaji pia ni mvuvi, na mchambuzi wetu anasema kwa ukanda wa Maziwa Makuu, mroaji ni mvuvi.