Madhara ya mabadiliko ya tabianchi yazidi kutwamisha hali za maskini duniani
17 October 2025

Madhara ya mabadiliko ya tabianchi yazidi kutwamisha hali za maskini duniani

Habari za UN - Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

About
Takribani watu milioni 887 duniani ambao ni maskini wanaishi kwenye maeneo yanayokumbwa moja kwa moja na madhara manne yasababishwayo na mabadiliko ya tabianchi ambayo ni joto kali, mafuriko, ukame na uchafuzi wa hewa, imesema ripoti mpya iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo, UNDP kwa kushirikiana na wadau. Ripoti inaonesha bayana kuwa hali hiyo inazidi kutwamisha watu hao kwenye hali tete zaidi. Assumpta Massoi amepitia ripoti hiyo na kuandaa taarifa hii.