
13 July 2026
IMO yatetea uhuru wa usafiri wa majini, sheria za kimataifa na usalama wa mabaharia
Habari za UN - Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu
About
Taarifa iliyotolewa leo na Shirika la Umoja wa Mataifa la Usafiri wa Baharini (IMO) imeeleza kuwa Baraza la shirika hilo lililohitimisha kikao chake cha 137 linasisitiza tena umuhimu wa kulinda haki na uhuru wa usafiri katika maji kwa mujibu wa sheria za kimataifa. Anold Kayanda ameifuatilia taarifa hiyo.