
01 October 2025
Angelique Kidjo, Mwanamuziki, asimulia safari yake ya elimu akiunga mkono wito wa UNICEF kwa viongozi wa Afrika
Habari za UN - Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu
About
Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto, UNICEF linatoa wito kwa viongozi wa Afrika kufanya uwekezaji wa kifedha wa busara utakaowezesha watoto kupata ujuzi wa msingi wa kujifunza na mustakabali wenye nguvu kwa bara la Afrika. Balozi Mwema wa UNICEF, Angelique Kidjo, katika kuunga mkono wito huo anasimulia safari yake kutoka kujifunza alfabeti hadi kuimba kwa ulimwengu mzima. Anold Kayanda anaeleza zaidi.