About
Katika Jarida la Habari za Umoja wa Mataifa hii leo Flora Nducha anakuletea-Leo WHO imefanya mkutano wa pili wa kamati ya dharura ya kanuni za afya za Kimataifa mjini Geneva Uswisi kutathmini kuhusu mlipuko wa virusi vya Ebola aina ya Bundibugyo nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC.-WHO pia imezungumza na waandshi wa habari DRC katika jitihada za kupambana na Ebola na pia kuhakikisha jamii inashirikishwa ipasavyo ikiwemo waendesha pikipiki au boda boda-Ripoti mpya iliyotolewa leo na WHO na UNICEF, imeonesha kuwa licha ya maendeleo yaliyopatikana katika muongo mmoja uliopita, vituo vingi vya afya duniani bado havina huduma za kutosha za maji, vyoo na usafi.-Katika mada kwa kina leo utamsikia Emmanuel Madragule muhudumu wa kibinadamu Bunia DRC anayefanya kazi na OCHA akieleza kinachumsukuma kuendelea kutoa huduma ya kibinadamu-Na katika jifunze Kiswahili utasikia maana ya neno "KARAKARA"