
08 December 2025
Australia kupiga marufuku mitandao ya jamii kwa walio chini ya umri 16
SBS Swahili - SBS Swahili
About
Kuanzia Jumatano wiki hii, Australia itakuwa nchi ya kwanza duniani kupiga marufuku watu walio chini ya umri wa miaka 16 kuwa na akaunti za mitandao ya kijamii, na kusababisha majukwaa makuu kufuata sheria hiyo au kukabiliwa na faini ya hadi dola milioni 50. Serikali ya Albanese inasema hatua hiyo inalenga kuwalinda vijana dhidi ya athari mbaya za mtandao na athari hasi za afya ya akili. Wazazi wengi wanaunga mkono mabadiliko haya, ilhali wakosoaji wanaonya kwamba vijana wenye ufahamu mzuri wa teknolojia wanaweza kupata mbinu za kuzunguka hatua hizi.