zeno
Create a Station
Explore
Religious
Music
News
Podcasts
Bible
By Genre
By Location
By Language
Download App
Toggle Sidebar
zeno
United Nations
Habari za UN - Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu
Daily News
Swahili
Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu
Website
Episodes
100
26 March 2026
JIFUNZE KISWAHILI - NENO: NYAPANYAPA
Sasa umewadia wasaa wa kujifunza Kiswahili hii leo, mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri Mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA. Anafafanua maana ya neno "NYAPANYAPA" katika muktadha wa uwindaji.Bwana Sigalla anasema "nyapanyapa ni tabia ya mwindaji ambayo anatembea kwa kunyata sana, pole pole ili asisikike wakati anawinda.Anakuwa ananyemelea. Lengo ni kuhakikisha...
26 March 2026
26 MACHI 2026
Hii leo jaridani tunamulika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, (DRC), hali Mashariki ya Kati, Amerika ya Kati, kilimo cha migomba kinachohimili mabadiliko ya tabianchi huko Pemba, Zanzibar nchini Tanzania na katika kujifunza lugha ya Kiswahili ni uchambuzi wa neno, 'Nyapanyapa.'MUHTASARIMabaraza ya Umoja wa Mataifa lile la Usalama na lile la Haki za Binadamu kwa nyakati tofauti yajadili hali ya...
9 min
25 March 2026
Tanzania: FAO na wadau 'wawanoa' maafisa misitu ili kudhibiti uvunaji haramu wa mazao ya misitu
Nchini Tanzania kunafanyika mafunzo kwa maafisa wa misitu yenye lengo la kulinda misitu, mafunzo yanayotekelezwa kwa pamoja na shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo, (FAO) na serikali ya Tanzania kwa ufadhili wa Muungano wa Ulaya (EU) kupitia mradi wa CookFund.Tweet URLMratibu wa Mradi kutoka FAO Diomedes Kalisa akizungumza kwa niaba ya Mwakilishi Msaidizi wa FAO Tanzania, Charles...
2 min
25 March 2026
Meli zilizokuwa zikipita Hormuz zilikuwa 129 kwa siku, sasa ni 2 hadi 7 kwa siku: UNCTAD
Tangu kuanza kwa vita huko Mashariki ya Kati baada ya Israel na Marekani kuishambulia Iran mnamo tarehe 28 Februari na kisha Iran kujibu mashambulizi, wasiwasi umekuwa ukiongezeka kuhusu kupanda kwa bei za mafuta na bidhaa nyingine. Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo na Biashara UNCTAD linafuatilia kwa karibu hali inayoendelea na kutoa takwimu na uchambuzi ili kuzisaidia serikali na wadau...
3 min
25 March 2026
Azimio lapitishwa kutambua biashara ya utumwa kupitia bahari ya Atlantiki ni uhalifu mkubwa dhidi ya binadamu
Umoja wa Mataifa leo umekuwa na tukio la kumbukizi ya siku ya kimataifa ya kukumbuka waathiriwa wa biashara ya utumwa kupitia bahari ya Atlanitiki ambapo nchi 123 wanachama wa Umoja huo wamepitisha azimio lililoandaliwa na mataifa 58 kutambua usafirishaji wa watu wa kiafrika na utumwa kwa misingi ya rangi ya waafrika kuwa uhalifu mkubwa dhidi ya binadamu. Nchi hizo 123 ni pamoja na zile wanachama...
3 min
25 March 2026
25 MACHI 2025
Yaliyomo katika Jarida hili la habari za UNKauli za fidia na haki zatawala tukio la kumbukizi ya biashara ya utumwa kupitia bahari ya Atlantiki.UNCTAD: Meli zilizokuwa zikipita Hormuz zilikuwa 129 kwa siku, sasa ni 2 hadi 7 kwa siku.FAO Tanzania na wadau wawanoa maafisa misitu kudhibiti uvunaji haramu wa mazao ya misitu
11 min
24 March 2026
JIFUNZE KISWAHILI: METHALI
Hii leo katika kujifunza lugha ya Kiswahili, leo mchambuzi wetu Dkt. Josephat Gitonga, ambaye ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi nchini Kenya, kwenye kitivo cha Tafsiri na Ukalimani anafafanua maana ya methali “Ateteaye mtuku ni tanguko la bure."Dkt. Gitonga anasema, "Mtuku ni mtu asiyefaa au asiyeweza kutegemeeka. Methali hii ina maana kwamba mtu asiyetegemeeka kamwe katika jamii na...
1 min
24 March 2026
24 MACHI 2026
Hii leo jaridani ni:Muhtasari;Mada kwa Kina na Jifunze lugha ya Kiswahili. Jarida leo linawasilishwa na Rashid Maleka kutoka Mwanza nchini Tanzania.Muhtasari wa Jarida:dadi ya vifo kutokana na shambulio dhidi ya hospitali moja huko Darfur, Sudan, Ijumaa iliyopita imeongezeka zaidi,Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi,UNHCR limetoa wito wa msaada wa haraka wa kimataifa ili...
10 min
23 March 2026
Furaha ni pale ninapoweza kuhudumia familia yangu
Katika kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Furaha ambayo huadhimishwa kila ifikapo tarehe 20 Machi, wakazi wa kata ya Luchelele, jijini Mwanza, kaskazini-magharibi mwa Tanzania, wameeleza maana ya furaha katika maisha yao ya kila siku, ambapo kwa wengi, furaha haitokani na anasa, bali inajengwa na afya njema, upendo wa familia, na uwezo wa kuitunza familia hiyo kwa mahitaji ya msingi. Wakizungumza...
2 min
23 March 2026
Fahamu jinsi serikali ya Kenya inasambaza visima vya maji kwa wananchi
Katika mazungumzo yafuatayo kati ya Anold Kayanda wa Idhaa hii na Hanna Wendot Cheptumo Waziri wa Jinsia, Utamaduni na Maslahi ya Watoto wa Kenya, Nchi hiyo ya Afrika Mashariki inajivunia kupiga hatua katika kuitatua changamoto hiyo. Waziri Hanna Wendot Cheptumo anaeleza kwamba Kenya kupitiua mfuko ilioupa jina NGAAF yaani National Government Affirmative Action Fund, mfuko wa fecha mahususi...
3 min